Rwanda: Mvua yaua watu 15 wiki mbili
![](IMG/logo/arton148414.jpg?1718225261)
Mvua kali inayonyesha nchini Rwanda imewaua takriban watu 15 katika siku 15, Wizara ya Majanga nchini Rwanda imesema.
Wananchi wanawoishi mahali pa hatari wameshauriwa kuhama kwa haraka.
Pia Rwanda imetangaza watu 22 walijeruhiwa, nyumba 200 ziliharibika pamoja na madaraja saba pia na barabara sita.
Nchi za mashariki mwa Afrika zinakabiliana na mvua nyingi mno siku hizi na kusababisha vifo vya watu 300 kwa ujumla.
Inatarajiwa kuwa mvua itaendelea kunyesha kwa wingi leo tarehe 9 Disemba 2019
Leave a Comment