Kiongozi Mkuu wa Iran, Ali Hosseini Khamenei, siku ya Ijumaa aliteua makamanda wapya wa jeshi kuchukua nafasi za waliouawa katika mashambulizi yaliyofanywa na Israel dhidi ya nchi hiyo.
Makao Makuu ya Kijeshi ya Iran yaliyoko mjini Tehran ni miongoni mwa maeneo yaliyolengwa katika mashambulizi ya alfajiri ya Ijumaa hii.
Waliofariki ni pamoja na Meja Jenerali Hossein Salami, aliyekuwa Kamanda Mkuu wa Vikosi vya Iran, na Meja Jenerali Mohammad Bagheri, aliyekuwa Kamanda wa Vikosi vya Ardhi.
Baada ya vifo vyao, jeshi la Iran lilitangaza kuwa Khamenei amemteua Meja Jenerali Mohammad Pakpour kuwa Kamanda Mkuu mpya wa Vikosi vya Iran, na Meja Jenerali Seyyed Abdolrahim Mousavi kuwa Kamanda wa Vikosi vya Ardhi.
Kiongozi Mkuu huyo alisema anawaamini maafisa wapya kuwa watalipiza kisasi kwa ajili ya wenzao waliouawa, na kuhakikisha kuwa Israel inalipa gharama ya vitendo vyake.


