diddy-legal

Majaji Wakwama Kwa Shtaka Kuu Linaloweza Kufunga Diddy Maisha Jela

Sangiza iyi nkuru

Majaji katika kesi ya Sean “Diddy” Combs bado wako kwenye mvutano baada ya kutangaza kuwa wameshindwa kukubaliana kuhusu shtaka kuu la jinai, ambalo linaweza kusababisha kifungo cha maisha jela.

Katika jiji la New York, mahakama kuu ilielezwa kuwa baraza la majaji 12 lilifikia uamuzi kwa mashtaka manne kati ya matano, lakini wameshindwa kuelewana kuhusu shtaka la tano, ambalo ndilo lenye uzito zaidi. Uamuzi huu wa awali ulitangazwa Jumanne jioni.

Sean Combs, mwenye miaka 55, amekanusha mashtaka yote, yakiwemo usafirishaji wa binadamu kwa ajili ya ngono, kuwaleta watu kwenye biashara ya ukahaba, na uhalifu wa mtandao wa kihalifu (racketeering).

Kesi hiyo imechukua miezi miwili, na imesikiliza ushahidi kutoka kwa mashahidi 34, wakiwemo wanawake waliokuwa washirika wa kimapenzi wa Diddy, wafanyakazi wa zamani, wanaume waliokuwa makahaba, na walinzi wa usalama.

Jaji Arun Subramanian amewataka majaji kuendelea kujadiliana ili waweze kufikia uamuzi wa pamoja. Waendesha mashtaka wameomba kutumika kwa “Allen charge”, ambayo ni agizo maalum linalowahimiza majaji wasiende hadi watakapofikia uamuzi mmoja.

Shtaka la uhalifu wa mtandao wa kihalifu (racketeering) linahitaji ushahidi wa walau vitendo viwili vya kihalifu vilivyopangwa na watu wawili au zaidi kwa muda mrefu. Waendesha mashtaka wamesema kuwa hili ndilo shtaka tata zaidi.

Diddy – anayejulikana pia kama Puff Daddy, P. Diddy, Love au Brother Love – ni msanii mashuhuri, mjasiriamali, na mwanamitindo, aliye na ushawishi mkubwa katika muziki na biashara.

Kesi inaendelea leo Jumatano, na huenda ikaendelea hadi Alhamisi, ingawa siku hiyo ni sikukuu ya Kitaifa ya Marekani – July 4th (Independence Day).

Soma Izindi Nkuru

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *