Baadhi ya wabunge kutoka jimbo lililokumbwa na mzozo la Kivu Kaskazini katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wanamtaka Rais Felix Tshisekedi kufikiria kuwashirikisha waasi wa M23 .
Katika barua ya wazi, wabunge hao walisema suluhu ya amani itapunguza mzozo unaoendelea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambao umesababisha mamia kwa maelfu kuwa wakimbizi katika mwaka uliopita.
Wabunge hao wamedai kuhusika katika mipango ya amani inayolenga kutatua mzozo wa usalama katika eneo hilo.
Wanataka njia za kibinadamu na barabara zilizofungwa katika maeneo yaliyoathiriwa na migogoro zifunguliwe.
Katika wiki za hivi karibuni, M23 imeteka vijiji na miji kama wanajaribu kusonga mbele kuelekea mji mkuu wa mkoa, Goma.
Kundi hilo liliratibiwa kuanza kujiondoa katika nyadhifa walizokuwa wakishikilia katika mashambulizi ya hivi majuzi kuanzia Jumanne kwa muda wa mwezi mmoja. Haijabainika ikiwa waasi wametii mpango wa kurudi nyuma.
Kundi la M23 limehusisha vikosi vya serikali katika mapigano makali kwa muda mwingi wa Februari.
Jopo la wataalamu wa Umoja wa Mataifa linasema kuwa M23 inaungwa mkono na Rwanda, jambo ambalo Kigali inakanusha.


