DRC: Wanajeshi wa Burundi watakaowekwa katika mhimili wa Sake, Kilolirwe, Kitchanga wawasili Goma

Sangiza iyi nkuru

Wanajeshi 30 wa Burundi walitua katika uwanja wa ndege wa Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Jumapili ili kujiunga na kikosi cha kimataifa kinachosaidia Kinshasa kukabiliana na ongezeko la wanamgambo katika eneo hilo. Wengine 70 walijiunga nao jioni kupitia mpaka wa Rwanda na Kongo wa Grande Barriere .

Wanajeshi hao watatumwa kama sehemu ya kikosi cha kikanda kilichoundwa na nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kujaribu kukomesha uasi wa M23 na kusambaratisha makundi mia moja yenye silaha ambayo yanakabili mashariki mwa DR Congo. Nchi saba za EAC zilituma wanajeshi mwishoni mwa mwaka jana katika eneo hilo.

Askari hawa watawekwa kwenye mhimili wa Sake, Kilolirwe, Kitchanga kwa mujibu wa Jenerali Kaputa, wa pili katika uongozi wa kikosi cha EAC.

Mapigano katika jimbo la Kivu Kaskazini yamesababisha idadi kubwa ya watu kuyahama makazi yao na kuzidisha hali ya wasiwasi, huku serikali ya DRC ikiishutumu Rwanda kwa kuunga mkono M23, madai yaliyokanushwa na Kigali lakini yakiungwa mkono na Marekani na mataifa kadhaa ya Magharibi.

Wanamgambo hao waliibuka tena kutoka katika hali ya utulivu mwishoni mwa 2021, na baadaye kumiliki maeneo mengi ya Kivu Kaskazini, ikiwa ni pamoja na sehemu kubwa ya eneo la kaskazini mwa mji mkuu wake Goma.

Soma Izindi Nkuru

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *