Raia wa Ujerumani alipatikana ameuawa nyumbani kwake Olodokilani Kajiado Magharibi nchini kenya .
Mwili wa Wilko Milicinovic, 80, ulipatikana kwenye dimbwi la damu Jumanne na mfanyakazi wake, polisi walisema.
Mwili ulikuwa umefungwa kwenye kitanda chake. Jicho lake la kushoto lilikuwa limeng’olewa na alikuwa na majeraha makubwa kichwani.
Polisi walisema wauaji hao walivamia nyumba yake na kuiba laptop yake.
Marehemu aliishi peke yake na alisaidiwa na mfanyakazi ambaye aliripoti kazini saa 8 asubuhi na kuondoka saa 5 usiku.
Mwanawe na binti-mkwe wanaishi katika nyumba tofauti ndani ya boma moja.
Mfanyikazi huyo, Ndetia Matambashi, aligundua mara ya kwanza madoa ya damu kwenye mlango wa mgeni huyo mnamo Jumanne, Machi 14, kabla ya kumjulisha binti-mkwe wa marehemu, Mary Nyambura.
Baada ya kukimbilia nyumbani kwa baba mkwe saa 10 alfajiri, akifuatana na maafisa wa polisi, Nyambura aligundua mzee huyo alikuwa ameuawa.
Polisi wanashuku kuwa Wilko alishambuliwa Jumatatu usiku, Machi 13.
Polisi walisema watu wasiojulikana waliingia nyumbani kwake kwa kuvunja mlango wa nyuma na, baada ya hapo, walimuua Wilko.
Sebuleni, kulikuwa na madoa kadhaa ya damu, ikionyesha kuwa Wilko anaweza kuwa alijitahidi kujinasua kutoka kwa wauaji wake.
Mwili huo ulipelekwa katika chumba cha maiti cha Hospitali ya Rufaa ya Kaunti ya Kajiado huku uchunguzi ukiendelea.
Hakuna aliyekamatwa hadi sasa.
Msemaji wa polisi wa kitaifa Dkt Resila Onyango alisema bado hawajabaini nia ya tukio hilo.
The Star


