1740138483767-824551740138503

Liverpool Yakutana na PSG Katika Raundi ya 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya

Sangiza iyi nkuru

Ijumaa hii, tarehe 21 Februari 2025, droo ya raundi ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya ilifanyika mjini Nyon, Uswizi, ikitangaza mechi zitakazopigwa katika hatua hii ya mtoano ya mashindano makubwa ya vilabu barani Ulaya.

Katika droo hii, Liverpool ilipangwa kucheza dhidi ya Paris Saint-Germain (PSG), mchezo unaotarajiwa kuwa mkali kutokana na historia kubwa ya vilabu hivi kwenye Ligi ya Mabingwa.

Mechi nyingine zilizopangwa ni:

  • Club Brugge vs Aston Villa
  • Real Madrid vs Atletico Madrid
  • PSV Eindhoven vs Arsenal
  • Benfica vs FC Barcelona
  • Borussia Dortmund vs Lille
  • FC Bayern Munich vs Bayer Leverkusen
  • Feyenoord vs Inter Milan

Ratiba ya Mechi:

  • Mechi za kwanza: 4-5 Machi 2025
  • Mechi za marudiano: 11-12 Machi 2025

Katika robo fainali, mshindi kati ya PSG na Liverpool atakutana na mshindi kati ya Club Brugge na Aston Villa. Kadhalika, mshindi kati ya Arsenal na PSV Eindhoven atacheza dhidi ya mshindi wa pambano kati ya Real Madrid na Atletico Madrid.

Robo Fainali:

  • Mechi za kwanza: 8-9 Aprili 2025
  • Mechi za marudiano: 15-16 Aprili 2025

Nusu Fainali:

  • Mechi za kwanza: 22-30 Aprili 2025
  • Mechi za marudiano: 6-7 Mei 2025

Fainali:

  • 31 Mei 2025 mjini Munich, Ujerumani

Mashindano haya yanaendelea kuvutia mashabiki wa soka, wakisubiri kwa hamu mechi kali za hatua zinazofuata.

Soma Izindi Nkuru

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *