Cristiano Ronaldo, raia wa Ureno, ameongoza tena orodha ya wanamichezo wanaopata mapato makubwa zaidi duniani, kwa mujibu wa jarida la Forbes. Hii ni mara ya tatu mfululizo na ya tano katika maisha yake ya kisoka.
Baada ya kujiunga na timu ya Al-Nassr nchini Saudi Arabia, Ronaldo alipata jumla ya dola milioni 275, zikiwemo milioni 60 kutoka kwenye mshahara wake wa uwanjani na milioni 215 kutoka kwenye mikataba ya kibiashara na mashabiki wake zaidi ya milioni 900 mitandaoni.
Stephen Curry wa Golden State Warriors alishika nafasi ya pili na dola milioni 156, akifuatiwa na bondia Tyson Fury aliyepata milioni 135, ingawa alinyang’anywa mataji yake na Oleksandr Usyk.
Mchezaji wa mpira wa miguu wa Marekani Dak Prescott alishika nafasi ya nne, Lionel Messi wa Inter Miami akawa wa tano, na LeBron James wa Los Angeles Lakers wa sita.
Juan Soto kutoka timu ya New York Mets (baseball) alishika nafasi ya saba kwa milioni 114, Karim Benzema wa Al Ittihad wa nane, Shohei Ohtani (baseball) wa tisa, na Kevin Durant wa Phoenix Suns alikamilisha Top 10 ya 2025.


