68887

FARDC Yaituhumu M23 kwa Mauaji ya Raia Walungu

Sangiza iyi nkuru

Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (FARDC) limeituhumu muungano wa AFC/M23 kwa kuwaua raia 17 siku ya Jumapili, tarehe 22 Juni 2025, majira ya saa 12:30 jioni, katika kijiji cha Munzinzi, cheo cha Ngweshe, eneo la Walungu, mkoa wa Kivu Kusini.

Katika taarifa iliyotolewa siku ya Jumatatu, tarehe 23 Juni 2025, FARDC iliongeza kuwa nyumba nyingi zilichomwa moto, na raia waliingiwa na hofu kubwa wakalazimika kukimbilia katika kambi za kijeshi zilizokuwa karibu kutafuta usalama.

Taarifa hiyo iliyosainiwa na msemaji wa FARDC, Jenerali Sylvain Ekenge, ilisema:
“Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo linashutumu vikali mauaji haya na linatoa wito kwa wananchi kuwa macho.”

Kwa mujibu wa FARDC, raia walilengwa na adui (AFC/M23) kwa tuhuma za kushirikiana na jeshi la serikali pamoja na wapiganaji wa kujitolea wa Wazalendo.

Tangu mwishoni mwa wiki iliyopita, taarifa kutoka kwa vyanzo vya karibu na serikali zinasema kuwa mapigano makali yameripotiwa karibu na Bukavu, ambako FARDC inaituhumu AFC/M23 kwa kushambulia ngome zao.

GuCgmEBXAAAIlNF

Taarifa hii ya FARDC imekuja siku moja tu baada ya AFC/M23 kutoa taarifa yake, ikikana tuhuma na kusema kuwa kuna propaganda zinazolenga kuichafua. Badala yake, AFC/M23 imeituhumu serikali ya Kinshasa kwa kuwatendea raia uhalifu wa kutisha, ikiwa ni pamoja na vitendo vya ulaji wa nyama ya binadamu vinavyofanyika hadharani.

Soma Izindi Nkuru

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *