Rais Paul Kagame amemfukuza kazi Naibu Kamishna wa Magereza (ACP) Dkt. George Ruterana pamoja na wengine 218 kutoka Mamlaka ya Magereza ya Rwanda (RCS).
Dkt. Ruterana alikuwa Mkuu wa Idara ya Afya katika RCS.
RCS imethibitisha kuwa yeye pamoja na wenzake wamefutwa kazi na Kiongozi wa Taifa, ingawa sababu ya kufukuzwa haikufafanuliwa.
Taarifa rasmi pia inasema kuwa wafanyakazi wanane wamewekwa tena katika maisha ya kiraia na wawili wakaachishwa kazi.
Rais Kagame pia amewastaafisha maafisa wakuu wakiwemo Kamishna wa Magereza John Bosco Kabanda, aliyekuwa Mkuu wa Divisheni ya Elimu ya Kiraia, pamoja na ACP Camille Gatete, Mugisha Munana Salim na Rutayisire Nshoza Emmanuel.
Pia, maafisa wakuu 10, maafisa wadogo 14, pamoja na maskari 60 wamewekwa katika mapumziko ya ustaafu.
Mbali na waliofukuzwa na kustaafu, maafisa kadhaa wa RCS wamepandishwa vyeo.
Miongoni mwao, CSP Moses Ntawiheba, John Dusa na Kamugisha Michael wamepandishwa kuwa ACP.
SSP Béatrice Uwamahoro, Olive Mukantabana, Jean Pierre Olivier Bazambanza na Sengabo Emmanuel Hilary wamepandishwa kuwa CSP.
SP Mukeshimana Marie Rose, Butare Godfrey, Ntakirutimana Eric, Mukeshimana Mwizerwa Dative, Niyindora Théoneste, Bugingo Janet, Ishimwe Emmanuel, Mbarushimana Alain Gilbert, Mugisha Alex Celestin, Muragizi Patrick na Ntwari Rémy wamepandishwa kuwa SSP.
Kwa maafisa wadogo, watatu walipandishwa kuwa SP kutoka CIP, na kumi wakawa IP kutoka AIP.
Kwa upande wa askari wa kawaida, sergeant 62 wamekuwa senior sergeant, corporal 20 wamekuwa sergeant, na warder 77 wamepandishwa kuwa corporal.


