Jumanne, tarehe 3 Juni 2025, Waziri wa Sheria, Constant Mutamba, anatarajiwa kufika mbele ya Ofisi ya Mwendesha Mashtaka Mkuu katika Mahakama ya Rufaa, kulingana na wito rasmi uliotumwa siku ya Jumatatu, tarehe 2 Juni.
Wito huu umetolewa kufuatia uamuzi wa Bunge la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kuruhusu mahakama kuanzisha uchunguzi dhidi ya Waziri wa Sheria.
Waziri Constant Mutamba anatuhumiwa kufuja takriban dola milioni 20 za Kimarekani, zilizotoka katika hazina ya taifa. Fedha hizo zilikuwa zimepangwa kujenga Gereza Kuu la Kisangani, mji mkuu wa Jimbo la Tshopo.

