Kamanda Mkuu wa Jeshi la Uganda, Jenerali Muhoozi Kainerugaba, amekemea vikali Jeshi la Ulinzi la Kenya (KDF), akisema kuwa Jeshi la Congo (FARDC) ni mara kumi bora zaidi kuliko KDF.
Kupitia chapisho kwenye ukurasa wake wa X, Jenerali Muhoozi alisema:
“Lazima niseme kuwa jeshi la Congo (FARDC)… licha ya changamoto kadhaa… ni bora mara 10 kuliko jeshi la Kenya (KDF).”
Alikosoa vikali Kenya kwa kushindwa kuwafukuza magenge yanayodhibiti mji mkuu wa Haiti, Port-au-Prince, licha ya kuwa na vikosi maalum huko.
Akaongeza:
“Kudhibiti Port-au-Prince kwetu ni kazi ya mwezi mmoja. Wakenya wameshindwa kwa karibu miaka miwili… na hiyo ndiyo tulitarajia. Ni waoga.”
Jenerali Muhoozi pia alitoa wito kwa Umoja wa Mataifa (UN) kuikabidhi UPDF (Jeshi la Wananchi la Uganda) jukumu la amani Haiti, akisema wana uwezo mkubwa kuliko Wakenya.
Katika ujumbe mwingine, aliwataka wanajeshi maalum wa Kenya walioko Port-au-Prince kurejesha utulivu ndani ya mwezi mmoja, la sivyo, UPDF itaingilia kati.


