11int-safrica-afrikaner-HFO-gqjc-articleLarge

Mara ya Kwanza: Weupe wa Afrika Kusini Wapewa Hifadhi ya Kisiasa, Wasafirishwa Marekani

Sangiza iyi nkuru

Wazungu wa kwanza wa Afrika Kusini waliopatiwa hadhi ya ukimbizi kupitia mpango ulioanzishwa na Rais wa Marekani, Donald Trump, kwa madai ya ubaguzi, waliondoka Johannesburg Jumapili hii, Mei 11, 2025, kuelekea Marekani.

Mwandishi wa shirika la habari la Reuters aliripoti kuwa alishuhudia mstari wa abiria weupe wakiwa na mizigo yao wakisubiri pasi zao kupigwa muhuri kabla ya kuingia kwenye eneo la kungojea ndege.

Msemaji wa Wizara ya Usafiri ya Afrika Kusini, Collen Msibi, alisema kuwa ndege iliyoandaliwa na Marekani ilikuwa na abiria 49.

Msibi alithibitisha kuwa waliokuwa wakihamia Marekani kama wakimbizi ni waafrika wa kizungu wa jamii ya Afrikaner, kundi la kikabila lenye asili kutoka kwa Wa-Dachi, Wajerumani na Wafaransa. Afrikaners waliongoza Afrika Kusini wakati wa utawala wa ubaguzi wa rangi (apartheid) uliowabagua vikali Waafrika Weusi.

Afrikaners wanawakilisha takribani 60% ya wazungu wa Afrika Kusini, wakati wazungu kwa ujumla ni asilimia 7 ya watu wote nchini humo.

Hata hivyo, licha ya kuwa wachache, bado wanamiliki takribani 78% ya ardhi ya kilimo nchini humo na utajiri wao ni mara 20 zaidi ya ule wa watu weusi.

Soma Izindi Nkuru

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *