imageresize

Serikali ya Senegal Yasitisha Mradi wa Akon City kwa Sababu ya Ucheleweshaji na Ukosefu wa Fedha

Sangiza iyi nkuru

Serikali ya Senegal imetangaza kuwa imesitisha kabisa mradi wa “Akon City”, uliokuwa ukiongozwa na mwanamuziki maarufu duniani, Akon, kutokana na ucheleweshaji mkubwa na ukosefu wa fedha zilizohitajika.

Mradi huo wa jiji la kisasa ulikuwa umepangwa kujengwa Mbodiène, kwenye pwani ya Atlantiki, na ulikuwa na lengo la kulifanya eneo hilo kuwa jiji la kiteknolojia la kisasa, kama lilivyoonyeshwa kwenye filamu ya Wakanda (Marvel).

Mnamo mwaka 2020, Akon alipewa hekari 136 za ardhi, lakini hadi sasa hakuna ujenzi mkubwa uliokuwa umeanza.

Mnamo Agosti 2024, alipewa onyo la mwisho kuanza ujenzi au kupokonywa ardhi. Kwa kuwa hakuna hatua iliyochukuliwa, serikali imeamua kuchukua tena ardhi hiyo.

Badala ya kujenga Akon City, serikali sasa itajenga kituo cha kisasa cha utalii chenye thamani ya dola bilioni 1.2, ambacho kinatarajiwa kuajiri watu takriban 15,000.

Akon sasa ameruhusiwa tu kubaki na hekari 8 kwa ajili ya mradi mdogo ukilinganisha na ule wa awali aliokuwa amepanga.

Soma Izindi Nkuru

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *