174866616410543a7eaa6eed64d41acc7df38f3eeb6f0_502999067_17847059574484705_3627736920994996518_n

Straika wa APR FC Azawadiwa Gari Jipya kwa Msimu wa Kipekee Uganda

Sangiza iyi nkuru

Mshambuliaji wa APR FC, Denis Omedi, ametunukiwa tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka kwenye Ligi Kuu ya Uganda baada ya kuonyesha kiwango cha juu akiwa na Kitara FC, kabla ya kujiunga na Rwanda.

Shirikisho la Soka la Uganda (FUFA) limemzawadia gari jipya pamoja na shilingi milioni moja za Uganda.

Mbali na kuwa Mchezaji Bora wa Mwaka, Omedi alipiga bao bora zaidi la msimu na pia akaingia katika kikosi bora cha mwaka. Alikuwa anawania tuzo hiyo na wachezaji nyota kama Ssekiganda Ronald na Allan Okello.

Omedi pia ameitwa kwenye timu ya taifa ya Uganda, itakayocheza mechi za kirafiki dhidi ya Cameroon na Gambia mwezi Juni 2025.

174866616410543a7eaa6eed64d41acc7df38f3eeb6f0 502999067 17847059574484705 3627736920994996518 n 1 1748666174834WhatsApp Image 2025 05 30 at 22.16.44 1150x766 1 1748666192099WhatsApp Image 2025 05 31 at 01.05.54

 

Soma Izindi Nkuru

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *