Jumamosi iliyopita, viongozi walitangaza kuwa waasi wanaohusishwa na Dola ya Kiislamu (ISIS) waliwaua watu 66 katika mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Waasi kutoka kundi la ADF (Allied Democratic Forces) wanadaiwa kuwaua raia katika eneo la Irumu, karibu na mpaka wa Uganda.
Shambulio hilo limetokea wakati hali ya usalama katika mashariki mwa Congo ikiwa tete kutokana na mapigano kati ya serikali ya Kinshasa na waasi wa M23.
Jean Tobie Okala, msemaji wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa (MONUSCO) huko Ituri, alisema tukio hilo ni kama “umwagaji mkubwa wa damu“.
Katika taarifa aliyoituma kwa Associated Press, Okala alisema kuwa takriban raia 30 waliuawa kati ya Alhamisi na Ijumaa, tarehe 11 Julai, katika eneo la Walese Vonkutu, jimbo la Irumu, mkoani Ituri.
Kwa mujibu wa ripoti kutoka kwa mashirika ya kiraia, idadi ya vifo imeongezeka kutoka 31 hadi 66.


