20250606_11042

Hatua ya Amani: Tshisekedi na Mpinzani wake Fayulu Wakumbatiana kwa Mazungumzo ya Kitaifa

Sangiza iyi nkuru

Rais Félix Antoine Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) amekutana na kufanya mazungumzo na mwanasiasa wa upinzani Martin Fayulu.

Alhamisi, tarehe 3 Juni, Tshisekedi alimkaribisha Fayulu pamoja na ujumbe wake katika ofisi yake.

Fayulu alikuwa ameomba kukutana na Tshisekedi ili wazungumze kuhusu namna ya kuokoa DRC kutokana na migogoro inayotishia taasisi na uhuru wa taifa hilo.

Ni Fayulu aliyeomba mkutano huo, licha ya kuwa na uhasama wa muda mrefu na Tshisekedi kufuatia uchaguzi wa mwaka 2018, ambao Fayulu anadai aliibiwa ushindi wake.

Picha zilizotolewa na Ikulu ya DRC zinaonyesha Tshisekedi akimkumbatia Fayulu alipomkaribisha, kabla ya kumwambia: “Nimefurahi kukuona, tutazungumza kwa moyo wazi.”

Mazungumzo kati ya Tshisekedi na Martin Fayulu yalichukua takriban saa mbili.

Fayulu, kiongozi wa muungano wa LAMUKA, aliliambia vyombo vya habari baada ya mkutano huo kwamba alimtaka Tshisekedi akutane haraka iwezekanavyo na Maaskofu wa Baraza la Maaskofu wa Kikatoliki (CENCO) pamoja na Wachungaji wa Kanisa la Kristo Congo (ECC) ili kwa pamoja watatue matatizo ya taifa.

Akasema: “Nchi iko katika wakati mgumu sana. Tunashambuliwa kila upande. Tunahitaji umoja wa kitaifa. Nimekuja kumwambia hatuna suluhisho 36. Ni lazima tuwe wamoja.”

Akaongeza: “Kwa kuzingatia changamoto zetu zote – kijamii, kisiasa na kiusalama – jibu liko kwenye mazungumzo jumuishi ya kitaifa. Nilimwomba afanye kila awezalo akutane na maaskofu wa CENCO na wachungaji wa ECC, ili tupate mkataba wa maisha unaotakiwa.”

Rais Tshisekedi anasemekana alikubali kutoa jibu la haraka kuhusu ombi hilo.

Hii ilikuwa ni mara ya kwanza Fayulu kukutana na Tshisekedi, licha ya kuwa amekuwa akimshutumu mara kwa mara kwa kuiangamiza DRC na kuiuza kutokana na kutokuwa na uwezo wa kuiongoza.

Soma Izindi Nkuru

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *