Tume Kuu ya Lugha na Utamaduni nchini Rwanda, RALC imewashauri vijana kukoma kupiga magoti ili kuomba wasichana kama watakubali kufunga ndoa nao.
RALC imesema jambo hilo ni kinyume na desturi na pia mila za Rwanda.
“ Nawapinga mno wale wanaoiga magoti. Unaona mambo hayo katika vyombo vya habari bila familia kujua.” Amesema Dk. Nzabonimpa Jacques.
Tume hiyo, imewataka watumie mbinu za zamani za Wanyarwanda kuwashawishi wanawake.
Hata hivyo, vijana wamesema hufanya hilo kama ishara kumuheshimu msichana.
“ (…) Naona ni kumpa heshima msichana, lakini kuna wale amabo wanafanya hilo kwa kuwaiga wengine, naona kwamba msichana ndiye ambaye anastahili kunipia magoti kunipongeza kwamba nataka kumuoa.” Janvier Romeo Nshimiyimana ameambiza Ukwezi
Tume ya RALC imekosoa tabia hii wakati ambapo linafanyika kwingi nchini kama vile harusini, tamasha,viwanja vya michezo na mahali pengine.


