Jeshi la Rwanda limeanzisha upelelezi kwa wanajeshi wake watatu wanaoshtakiwa kuwabaka wanawake eneo la Bannyahe Mjini Kigali.
Habari zimezagaa kuwa wanajeshi hao walibaka wanawake na kuwapiga waume zao wiki iliyopita.
Msemaji wa Jeshi la Rwanda, Luteni Kanali Innocent Munyengango jana alisema upelelezi utaazishwa kuhusu mashtaka hayo.
Pamoja na hayo, kwa mujibu wa BBC, upelelezi umeanzishwa na wakazi wa eneo hilo wanatoa ushahidi wao.
Ni mala ya kwanza baadhi ya wanajeshi wa Rwanda kushtakiwa mambo ya ubakaji.
Isangize abandi
Tanga igitekerezo